tag:blogger.com,1999:blog-34889602030753033852024-03-12T18:44:07.166-07:00Kishindoleo Loves' FieldUnknownnoreply@blogger.comBlogger10125tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-2206821419004127142013-01-05T07:47:00.001-08:002013-01-07T15:34:24.933-08:00Mwanamke Unajua Stail hizi ebu angalia Video hii umshike mmeo <div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<iframe allowfullscreen="allowfullscreen" frameborder="0" height="360" src="http://www.youtube.com/embed/J-seD81a3kA?feature=player_detailpage" width="640"></iframe></div>
<iframe width="640" height="360" src="http://www.youtube.com/embed/HsdDkcZRFdc?feature=player_detailpage" frameborder="0" allowfullscreen></iframe>
<iframe width="640" height="360" src="http://www.youtube.com/embed/vMkHKZHcTh0?feature=player_detailpage" frameborder="0" allowfullscreen></iframe>
Unknownnoreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-71086498073674491682012-11-08T01:43:00.002-08:002012-11-08T10:13:03.017-08:00Je unajua Wanaume wanaweza kuwekwa Kiganjani<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://3.bp.blogspot.com/-oXbQoydew5k/UJt-QtE-h2I/AAAAAAAACmQ/A38x6ZbZnaw/s1600/lovers+smile.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="358" src="http://3.bp.blogspot.com/-oXbQoydew5k/UJt-QtE-h2I/AAAAAAAACmQ/A38x6ZbZnaw/s640/lovers+smile.jpg" width="640" /></a></div>
<br />
Kuna baadhi ya wanawake walioolewa ambao wamekuwa wakijiamini sana
kwamba hawawezi kusalitiwa eti wakidai kuwa, wamewaweka waume zao
viganjani.<br />
<br />
Maneno haya yaweza kuwa si mageni masikioni mwako. Huenda
ulishawahi kumsikia mwanamke akisema: ‘Mimi mume wangu hapindui kwangu,
nimemuweka kiganjani na hawezi kunisaliti kwani nampa kila kitu’.<br />
Maneno haya yana tafsiri nyingi. Anayesema haya inawezekana kajidanganya
kwa kwenda kwa waganga na kapewa vilimbwata, hivyo anaamini vitamfanya
mumewe asimsaliti.<br />
<br />
Mwingine anaweza kusema maneno hayo akimaanisha
kuwa, anampa mumewe mapenzi kinyume na maumbile wengine wanaita tigo hivyo hakuna kitu
ambacho anaweza kukifuata nje. Hii inatokana na ulimbukeni wa baadhi ya
wanawake kuwa, eti wanaume wengi wanatoka nje ya ndoa zao kufuata kitu
hicho.<br />
<br />
Labda nikuulize wewe mwanamke kwani hicho unachodai unampa wengine hawana? kama ni kinyume na maumbule hata ukimpa wewe kama ni wa kutoka nje anaweza kutoka na kudhani labda tigo ya nje ni nzuri zaidi. Kwani wanaotoka nje ya ndoa zao unadhani nini wanachokifuata ambacho wewe huna! usijidanganye na hatimaye ukamkosea Muumba wako bure.<br />
Naomba niwaombe enyi wanawake mnapenda mchezo huo acheni kwani ni hatari kwa afya zenu na pia hata vitabu vya dini vinakataza mchezo huo. Hiyo si dawa ya kumfanya mumeo asitoke nje ya ndoa.<br />
<br />
Leo ngoja niwape mbinu chache za kuwaweka waume zenu kiganjani.<br />
<br />
<b>Mpe mumeo anachohitaji </b><br />
Wanawake wengi wanashindwa kujua wao wanatofautiana na wanaume kwa hisia na hata mawazo ya mapenzi. Wanaume wana mambo wanayoyapenda kutoka kwa wake zao hasa katika masuala ya mapenzi. Kwanza wanawake wajue wanaume wengi wana hisia za haraka za kufanya mapenzi kuliko wanawake.<br />
<br />
Mwanaume alivyoumbwa ni kwamba akiona tu mfano mwanamke umevaa kanga moja au umevaa night dress hiyo inatosha kusisimua. Wapo wanawake wanaowasisimua waume zao bila wao kujua. Mfano umevaa tu kanga moja au night dress ndani huna kitu. Kwako ni jambo la kawaida lakini kwa mwanaume sio la kawaida kwa kukuona hivyo tayari unakuwa umeamsha hisia zake. Ukimwona anakuja kutaka haki yake usidhani anakusumbua. Ujue tayari mwenzako alishafiria mbali zamani we huna habari.<br />
<br />
Ni vyema ukawa mwangalifu kujua hisia za mwanaume huyo mumeo kama inawezekana mpe anachohitaji kwani usipofanya hivyo unamwathiri kisaikolojia na anaweza kufikiria nje. Wanawake wengi wa nje waliowaweka waume zenu kiganjani hiyo ndio mbinu wanayotumia. Akiwa na ahadi na mumeo atamkuta kanga moja au amevaa night dress na kila anachohiji atapewa haraka tena kwa madoido. Kwanini akitaka hayo hayo kwa mkewe hapewi je ana kosa gani anapofikiria nje?<br />
<br />
Sasa nikuulize wewe mwanamke umemsisimua mwenyewe kwa mwonekano wako unamnyima ya nini.<br />
<br />
<b>Mvutie mumeo kwa mwenekano wako</b><br />
Mvuto ni muhimu sana kwa mwanaume. Wanaume wanapenda wanawake wanaowavutia kihisia. Niwaambie wanawake mlioolewa jueni kumvalia mumeo mavazi yanayomvutia.<br />
Sio vibaya kama nilivyosema hapo juu ukavaa kanga moja kama upo pamoja nae. Kama nilivyoeleza hapo juu mwanaume anasisimka kwa kuona. Kwanini avaliwe kanga moja na wanawake wa nje wakati wewe unaweza kuvaa. <br />
<br />
Wanawake jueni hili mnapokuwa karibu na waume zenu jianchieni Kwa mfano hakuna ubaya wakati mumeo karudi kutoka kazini akiwa amechoka, wakati unampotengea chakula ukavaa kanga moja au night dress. Unaweza kuona hilo ni jambo dogo lakini kisaikolojia utakuwa umefanya jambo kubwa. Hapo hata kama atakuwa ameudhiwa kazini atasahau na kukuona wewe mpenzi wake.<br />
<br />
<b>Usafi panga vitu vyako vya chumbani vizuri</b><br />
Jambo hili limekuwa lizizungumzwa sana hadi wengine wanasema mwanamke usafi. Kisaikolojia mpangalio wa vitu ndani na hasa chumbani kama ni mbovu unaweza kuathiri hata tendo la ndoa. Kama chumba ni kichafu vitu havijapangwa vizuri kisaikolojia kunapunguza msisimko wa mapenzi na hata kumfanya mwenzako achukie kufanya na wewe tendo hilo ukadhani hakupendi.<br />
<br />
Mwanamke tandika kitanda chako vizuri panga chumba chako tandika shuka nzuri. Siku hizi kuna shuka zina maneno ya mapenzi nunua hiyo uwe unatandika. Kisaikolojia utamfanya mpenzi wako avutiwe chumba chako na hata wewe mwenyewe. Mazingira mazuri yatamfanya asisimke haraka kimapenzi anapokuwa na wewe na hata kuitamana nyumba yake na kurudi mapema nyumbani.<br />
<br />
Jinsi chumba kilivyo rafu ndiyo wanasakolojia wanasema kunafanya ubongo uwe rafu hata kuchukia. Unaweza kumwona mwenzako anachukia kumbe ni kutokana na mpangilio mbovu wa chumba ndio sababu inayomfanya achukie.<br />
<br />
<b>Uwe msafi wa mwili</b><br />
Sio usafi wa chumba pekee unatosha pia na usafi wa mwili wako ni muhimu. Niwakumbushe wanawake hakuna kitu kinachowachukiza wanaume kama mwanamke mchafu. Asiyejipenda. Sio lazima ujirembe sana lakini jitahidi ukawa msafi. Oga vizuri paka mafuta au lotion yako jipulizie manukato kidogo yanayomvutia mumeo. Sio lazima utumie gharama kubwa usafi wa kawaida unatosha.<br />
<br />
Nikwambie wanawake wa nje hawana zaidi ya hayo ni hayo hapo juu na mengine ndiyo wanayotumia kuwaweka waume zenu kiganjani. Usijaribu kwenda kwa mganga hakuna atakachokusaidia memeo atatoka kama wewe humsisimui, hupangi vitu vyako vizuri na pia kama unaendekeza uchafu ni rahisi mumeo kufikiria nje.<br />
<br />
Kujiamini kwako iwe ni kwa sababu unajua ‘kumhendo’
mumeo kwa kumpa mapenzi ya kiwango cha juu, kumheshimu, mjali na
kumpatia mambo ya msingi ambayo anastahili kuyapata kutoka
kwako. Ukifanya hivyo utaifanya roho yake imsute kila anapotaka
kukusaliti.<br />
<br />
Hiyo ndiyo iwe sababu ya wewe kujiamini na wala huna
sababu ya kujinadi kwa wenzako. Tambua kuwa kuna wanaofikia hatua ya
kuhatarisha maisha yao kwa kutoa ‘mtandao’ wakijua kuwa ni njia ya
kuwashika waume zao kumbe wanajitafutia matatizo makubwa.<br />
<br />
Wapo
waliopoteza fedha zao nyingi kwa kwenda kwa waganga ili waume zao
wasifurukute mbele zao lakini imekuwa kazi bure. Shituka leo, anza
kutumia mbinu sahihi za kuishikilia ndoa yako na usijidanganye kwa
kufanya mambo ambayo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.<br />
<br />
Mwanamke
aliyekamilika ni yule anayeuthamini mwili wake, sasa kwa nini leo hii
ukubali ‘kumrukisha ukuta’ mumeo ili kumfanya asiende nje? Kwa nini
utumie fedha zako kwenye kumtafutia limbwata mumeo wakati wewe mwenyewe
ni limbwata tosha?<br />
<br />
Leo inatosha niishie hapa tutaendelea siku nyingine. cheers! </div>
Unknownnoreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-11755957723948104892012-10-29T14:21:00.001-07:002012-10-29T14:39:22.258-07:00Je unajua ni hatari kumdadisi mpenzi wako alitembea na wangapi?<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://1.bp.blogspot.com/-uiin8wFJwVU/UI7v_siMq9I/AAAAAAAACGk/Mskn1pM-yPk/s1600/couples.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="480" src="http://1.bp.blogspot.com/-uiin8wFJwVU/UI7v_siMq9I/AAAAAAAACGk/Mskn1pM-yPk/s640/couples.jpg" width="640" /></a></div>
<br />
KATIKA mapenzi kuna mambo ambayo hayastahili kupewa muda wa kuyajadili.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba, mengine yanaweza kutibua furaha
iliyopo na kuweza kupindisha maisha yenu.<br />
<br />
Kwa kuthibitisha hilo,
sikia kisa hiki. Jamaa mmoja aliyefahamika kwa jina la Rashid
alibahatika kumpata mke mzuri sana aliyefahamika kwa jina la Wahida.
Yaani mwanamke ambaye kila mwanaume akimuona ni lazima atamani kuwa
naye. <br />
<br />
Baada ya mwanaume huyo kumuoa, waliishi kwa muda mrefu sana na
ndoa yao ilikuwa ikitawaliwa na furaha siku zote. Wakabahatika kupata
watoto wawili. Hakika mwanamke huyo alikuwa mke kwa maana halisi ya mke.
<br />
<br />
Alikuwa akimheshimu sana mumewe na kumpatia kila aina ya furaha.
Kwa kifupi ilikuwa ni ndoa ya kuigwa. Siku moja Rashid alikutana na
rafiki yake wa muda mrefu sana.<br />
<br />
Mazungumzo yao yalikuwa mengi lakini
ikafika mahali yule rafiki akamuuliza Rashid kama ameshaoa. Rashid
akajibu kuwa kamuoa msichana mmoja anayeitwa Wahida. Yule jamaa
akashangaa kusikia Rashid kamuoa Wahida, mwanamke ambaye siku za nyuma
alikuwa ni changudoa.<br />
<br />
Rashid aliposikia kuwa Wahida alikuwa
changudoa, ati akaumia sana na akaanza visa kwa mkewe na hatimaye
wakaachana. Akaoa msichana mwingine dogodogo kutoka kijijini ambaye
hajaguswa. Alichokiona kwenye ndoa yake hiyo ya pili alijuta hadi
akamkumbuka Wahida. <br />
<br />
Tunajifunza nini kwenye kisa hiki? Ni kwamba,
unapokutana na mpenzi wako kwa mara ya kwanza kuna mambo ya msingi
ambayo kiukweli unastahili kuyajua. Hapa namaanisha historia ya maisha
yake. Unapotaka kujua historia ya maisha ya mpenzi wako siyo lazima kila
kitu ujue. Mengine yaache abaki nayo kwani hata akikuambia hayawezi
kukusaidia kiviiile.<br />
<br />
Lipo hili swali la umeshwahi kutembea na
wanaume/wanawake wangapi hadi leo? Hili si zuri kumuuliza mpenzi wako.
Kwa nini nasema hivyo? Nina sababu mbili. Kwanza ni vigumu sana kupata
jibu la kweli, yaani tarajia kudanganywa. Hapo unaweza hata kuambiwa
hajawahi kuwa na mpenzi kumbe katika ukweli tangu ameyajua mapenzi,
ametoka nao zaidi ya kumi.<br />
<br />
Sababu nyingine ya kwa nini hustahili
kuuliza swali hilo ni kwamba, inaweza kukufanya ukabadili mawazo yako na
hata uhusiano wenu ukakomea hapo. Unaweza kukutana na msichana mzuri
sana mwenye kila sifa nzuri na katika historia yake ya mapenzi anaweza
kuwa ameshapita kwa wanaume kibao kiasi kwamba hata idadi amesahau.<br />
<br />
Sasa kama utamuuliza na yeye akawa mkweli kwako kwa kukujibu kuwa, ni wengi kiasi kwamba hata idadi hakumbuki, utajisikiaje?<br />
<br />
Hakika
unaweza kujikuta unanyong’onyea na kushangaa hata ile hamu ya kuendelea
kuwa naye inaisha licha ya kwamba hukustahili kuwa hivyo. Matokeo yake
unaweza kumkosa mtu ambaye alistahili kuwa na wewe na mkaishi maisha ya
raha mustarehe.<br />
<br />
<b>Kuwa na idadi kubwa ni tatizo?</b><br />
Kuna
mtaalam mmoja aliwahi kusema kuwa, katika maisha ya sasa hakuna
mwanamke anayeolewa akiwa na usichana wake na kama wapo ni wachache
sana. Akaeleza kuwa, msichana akishatolewa usichana wake hata akiwa
ametembea na wanaume ishirini hana tofauti na yule aliyetembea na wawili
tu.<br />
<br />
Mtaalam huyo akasema, tena inawezekana aliyetembea na wengi
akatulia kwenye ndoa yake kuliko yule aliyetembea na mmoja au hajaguswa
kabisa. Hapo ndipo inapoonekana kwamba, kuwa na historia ya kwamba
uliwahi kutoka kimapenzi na wanaume/wanawake wengi, hakuna madhara
makubwa katika ndoa. <br />
<br />
Ndiyo maana inashauriwa kulifutilia mbali swali
la kutaka kujua idadi ya wapenzi aliyowahi kuwa nao huyo mpenzi wako au
hata kuwajua kwa majina. Hii ni kwa sababu hata ukijua haitakusaidia
chochote zaidi ya kukuchanganya na kukufanya ukose imani kwa mpenzi
wako.<br />
<br />
kama utakuwa umenufaika usiwe mchoyo mwambie na rafiki yako naye asome safu hii kupitia <a href="http://www.kishindoleo.blogspot.com/">www.kishindoleo.blogspot.com</a><br />
<br />
Makala hii kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers </div>
Unknownnoreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-79711068503330554492012-10-28T12:55:00.004-07:002012-10-28T16:32:16.732-07:00 Pete ya Uchumba si Ndoa, Je mwanamke unajua hiyo ni nini?<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://3.bp.blogspot.com/-Ry8_Oqi9QFA/UI2NjhuQW7I/AAAAAAAACBc/CR-ptG-ehPM/s1600/Engagement+ring.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="426" src="http://3.bp.blogspot.com/-Ry8_Oqi9QFA/UI2NjhuQW7I/AAAAAAAACBc/CR-ptG-ehPM/s640/Engagement+ring.jpg" width="640" /></a></div>
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://3.bp.blogspot.com/-CY2na7Chgwo/UI2NkEXsYvI/AAAAAAAACBg/fBRFURJzxJg/s1600/ring-exchange.jpg" imageanchor="1" style="clear: right; float: right; margin-bottom: 1em; margin-left: 1em;"><img border="0" height="213" src="http://3.bp.blogspot.com/-CY2na7Chgwo/UI2NkEXsYvI/AAAAAAAACBg/fBRFURJzxJg/s320/ring-exchange.jpg" width="320" /></a></div>
Rafiki zangu leo tutajifunza kitu kipya kabisa. Naamini utabadili namna
ya kufikiri mara mada hii itapofika ukingoni. Nazungumzia kuhusu pete za
uchumba. Hizi zimekuwa maarufu sana katika jamii yetu siku hizi.<br />
<br />
Watu
wanakutana disko, wiki mbili baadaye wanavalishana pete! Tayari
ameshachumbiwa na amekuwa chini ya miliki ya mtu. Uko wapi usahihi wa
pete za uchumba? Vijana wamechanganyikiwa kwelikweli! Wanataka pete tu!<br />
<br />
Inawezekana
wewe msichana unayesoma mada hii sasa hivi umevaa pete ya uchumba au
pengine uko njiani kuvalishwa...vizuri! Lakini unaelewa nini kuhusu pete
ya uchumba? Unautumiaje uchumba wako na mpenzi wako?<br />
<br />
All About Love
pekee ndiyo mahali utakapoweza kutolewa matongotongo kuhusu suala la
pete. Nikuambie kitu? Usiniache please, twende pamoja tuone ukweli. <br />
<br />
NI NINI HASA?<br />
Linatokana
na neno la Kiingereza linaloandikwa engagement ring lenye maana
nyingine ya commitment ring. Kwa Kiswahili rahisi ni pete ya ahadi.
Msichana kuvalishwa pete ya uchumba, maana yake amevalishwa alama ya
ahadi.<br />
<br />
Jambo moja unatakiwa kusafiri nalo hapa ni kwamba, ahadi inaweza kutekelezwa au isitekelezwe. <br />
<br />
KUHALALISHA PENZI<br />
Awali
kulikuwa hakuna kabisa utaratibu huu wa pete za uchumba. Mvulana
akimpenda msichana, taratibu za kawaida zilifuatwa kwa maana ya posa na
baadaye mahari kisha ndoa. Hizi ni tabia za Kimagharibi ambazo zimekuja
hivi karibuni.<br />
<br />
Utaratibu huu umepokelewa vibaya (hasa na wasichana),
wengi wamekuwa na shauku sana pete. Imani yao ni kwamba ukivalishwa tu,
basi ndoa inanukia. Akipata mpenzi, anamlazimisha amvalishe pete.<br />
<br />
Kwani
kazi basi?! Aaah wapi! Jamaa anakwenda zake kwa Sonara anatengeneza
pete ya laki tatu anamvalisha baa! Tayari wachumba! Hakuna mzazi wala
mjomba anayejua. Hapo sasa ndiyo kwenye ukichaa – mwanamke atajiachia
vyovyote atakavyo kwa mwanaume huyo.<br />
<br />
Wanaume nao wanashangilia.
Tatizo si pete? Anakuvalisha halafu anakutumia kwa nafasi, akiridhika
anakuacha tena wengine huchukua na pete zao kabisa, halafu anatafuta
mwingine anamvalisha. Mchezo unaendelea.<br />
<br />
UCHUMBA SI NDOA<br />
Dada
zangu wapendwa fumbukeni macho, uchumba si ndoa. Utakuta mwanamke
amevalishwa pete ya uchumba, basi kishakuwa mke. Atakwenda kwa huyo
mwanaume, atafanya usafi, atafua, atapika na penzi atatoa!<br />
Mwanaume
anaridhishwa na kila kitu. Hapo unakuwa huna jipya tena. Hata kama
anakupenda kwa kiasi gani, hawezi kuwa na haraka ya ndoa, maana kila
kitu anachotakiwa kupata mwanandoa unampa!<br />
<br />
Ya nini ajisumbue? Ya nini
aanze kufikiria mambo ya vikao? Presha za nini? Haoni sababu na wakati
muda ukizidi kwenda, anaendelea kukuchoka na kutafuta mwingine
anayejitambua na kumuoa. Una lipi jipya utakalomwonesha ndani ya ndoa
wakati kila kitu tayari anakijua?<br />
Mabinti muwe makini. Kwa bahati
mbaya sana, siku hizi wanaume wanakimbia kuoa mapema, ukijirahisi kwa
pete utazivaa sana, lakini si ile ya madhabahuni. Utatumika na kuachwa.<br />
<br />
UCHUMBA HUVUNJIKA<br />
Acha
kujidanganya, uchumba si ndoa (ingawa zipo zinazovunjika kulingana na
ilipofungwa). Usiamini kuwa mchumba wa mtu basi kazi imeisha. Bado tena
kubwa sana. Usikubali akutumie anavyotaka kwa kigezo cha pete.<br />
<br />
Utakuta
msichana amejitunza kwa muda mrefu sana lakini akishavalishwa pete tu,
basi yupo tayari kwa lolote. Acha kujidanganya ndugu yangu. Endelea
kujifunza na yeye anapaswa aendelee kukuheshimu kwa sababu bado si mke
wake.<br />
Baadhi ya madhehebu ya dini hutangaza ndoa kwanza kwa waumini
kabla ya kufunga kwa sababu wanataka kupata uhakika wa wanandoa
watarajiwa. Hata kama kanisani wanajua, kesho bwana harusi akikataa
ndoa, hakuna wa kumlazimisha.<br />
Kikitokea kipingamizi kadhalika, ndoa haifungwi tena. Kuwa makini.<br />
<br />
UKWELI KUHUSU PETE<br />
Achana
na pete za kuvalishana uchochoroni. Mnavalishana pete gesti au kwenye
kumbi za starehe – siyo sawa. Pete sahihi ni ile ambayo msichana
atavalishwa mbele ya wazazi wa pande zote mbili, tena mahari ikiwa
imeshatolewa na tarehe ya ndoa inajulikana.<br />
<br />
Huu ndiyo usahihi na hapo
tutakubaliana na wewe kwamba umevalishwa pete ya uchumba na upo mbioni
kuolewa. Je, ukifikia hatua hiyo ndiyo ujiachie kwa mchumba wako? La
hasha! Tena hapo ndipo unapotakiwa kuonesha heshima zaidi.<br />
<br />
Kwamba
wewe ni mchumba wa mtu na wazazi wako wanafahamu. Kuonekana mkiwa pamoja
uchochoroni si kiashiria kizuri. Je Kuna mahali nimekuacha? Nakupenda
sana.<br />
<br />
Mwisho kabisa kama umefurahia na umejifunza kitu kupitia makala hii usiwe mchoyo mwambie na rafiki yako asome naye makala hii hapa kupitia <b> <a href="http://www.kishindoleo.blogspot.com/">www.kishindoleo.blogspot.com </a></b>kwa njia hiyo utakuwa umemsaidia asije akaingia mtegoni.<br />
<br />
Usiache kusoma ukurasa huu wa Mapenzi kuna mengi mazuri yanayokuja siku za usoni<br />
<br />
Chears!<br />
<br />
<b>Makala hii imeandikwa na Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya
Mapenzi anayeandikia Magazeti ya Global Publishers. Ameandika vitabu vya
True Love, Let’s Talk About Love na All About Love vilivyopo mitaani</b><br />
<br />
<b>Makala nzima ni kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers </b><br />
<br /></div>
Unknownnoreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-48577177359762131742012-10-25T16:13:00.001-07:002012-10-25T16:16:49.893-07:00Unajua Wanaume wanapenda kuoa Wanawake wa aina gani?<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://1.bp.blogspot.com/-VXGT5FLxc3U/UInHea8AD8I/AAAAAAAAB1Q/IEsexzg17dg/s1600/sexist+women.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="640" src="http://1.bp.blogspot.com/-VXGT5FLxc3U/UInHea8AD8I/AAAAAAAAB1Q/IEsexzg17dg/s640/sexist+women.jpg" width="426" /></a></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: Georgia,"Times New Roman",serif; text-align: left;">
</div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: Georgia,"Times New Roman",serif; text-align: left;">
</div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Habari
za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza
kunikutanisha na nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine
nazungumzia juu ya mada mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila
siku.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Wiki hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa. <a href="http://www.blogger.com/blogger.g?blogID=3755141742104169318" name="more"></a></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
</div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Wanaume
wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa
mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi
kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa
pamoja kwa kipindi chote cha maisha.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
</div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Wanawake
wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya
wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na
kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya
uzuri.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Hali
sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na
sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
</div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Utafiti
ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo,
kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo
ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa
kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu
kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><br />
</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> <b> </b></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><b>MWEYE MAPENZI YA KWELI</b></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Lengo
kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa
mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio
wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi
kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga.
Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama
kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya
dhati kutoka moyoni mwake. </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Mwanamke
asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho
yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona
anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya
kifedha mapenzi yanaanza kufifia.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Kwanini
wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao
na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba
maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda
na kushuka.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Sio
kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi
ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe
tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si
kwa kipindi fulani tu cha neema.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Si
hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha ya ndoa yanatawaliwa na
mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi
kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda
mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha
ya raha mustarehe.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><b>WENYE TABIA NZURI</b></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Tabia
njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda,
hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa
tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na
ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na
maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani
utaambiwa anatabia mbaya.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Naweza
kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya wanawake kukosa
wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao
nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Si
hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa
kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache
yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa
ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> <b> </b></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><b>WENYE UCHU NA MAENDELEO</b></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Hivi
karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa
hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'.
Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma
kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio
vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata
vijijini. </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Ile
dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa
akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati.
Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za
maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini
wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili
wafanikiwe.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><b>WASIOPENDA MAKUU</b></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Kuna
wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza
kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali
hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila
wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?"</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Akimuona
rafiki yake kanunua simu ya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na
mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace’. Ukienda naye Pub
anakuambia, "mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’.
Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na usipotekelezea
anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><br />
</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="clear: right; float: right; font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; margin-bottom: 1em; margin-left: 1em; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Wanawake
kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume
wa kuwaoa. Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume
atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila
atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune
mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au
leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi
nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu
fulani.’</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Wanaume
ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote
ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa tatizo. Kitu ambacho
kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa
bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Kuna
wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea
hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au
wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema. </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Sisemi
kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu
kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona
kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa
utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi
wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulani wakati
inawezekana uwezekano haupo.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><b>WAVUMILIVU</b></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Wapo
wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba
maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama
kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke
anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea
anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Wangapi
leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotea kuumwa, kufilisika ama
kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza
kuwafanya maisha yao kutingishika?</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">Uvumilivu
kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama
nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima
atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote,
yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi
wengependa kuwa nao maishani mwao.</span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"> </span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" id="yui_3_2_0_1_1342046182569112" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><span id="yui_3_2_0_1_1342046182569109">Licha
ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu,
wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo
kimsingi havikubaliki katka jamii.</span></span></div>
<div class="yiv234276477MsoNormal" id="yui_3_2_0_1_1342046182569112" style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;"><span id="yui_3_2_0_1_1342046182569109">Tabia
hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu
kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.</span></span></div>
<div style="font-family: "Helvetica Neue",Arial,Helvetica,sans-serif; text-align: left;">
<span style="font-size: large;">
Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa
wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali jijini Dar-es-Salaam.</span><br />
<span style="font-size: large;"><br />
</span><span style="font-size: large;"> Kwa
maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume
wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa
umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu,
chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja
hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.</span></div>
</div>
Unknownnoreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-7987561649990729592012-10-24T05:12:00.002-07:002012-10-24T05:12:21.496-07:00Mwanamke kuwa chini ya Mwanaume sio sababu ya kunyanyaswa<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"><tbody>
<tr><td style="text-align: center;"><a href="http://3.bp.blogspot.com/-H9YGJW4JlIY/UIfZOR1gCoI/AAAAAAAABwo/z8FGajRjA84/s1600/crying+woman.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"><img border="0" height="484" src="http://3.bp.blogspot.com/-H9YGJW4JlIY/UIfZOR1gCoI/AAAAAAAABwo/z8FGajRjA84/s640/crying+woman.jpg" width="640" /></a></td></tr>
<tr><td class="tr-caption" style="text-align: center;"><br /></td></tr>
</tbody></table>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://theindustrydude360.com/wp-content/uploads/2012/08/Black-couple-upset-scaled.jpg" rel="nofollow" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;" target="_blank"><br /></a></div>
<br />
LIPO jambo gumu katika ulimwengu wa uhusiano ambalo limekuwa tatizo
kubwa na fumbo linalowashinda wengi. Nazungumzia mwanamke kuwa chini ya
utawala wa mwanaume. Kwa ujumla ni jambo la kawaida kabisa.<br /><br />
Huu ni
msingi uliojengwa tangu zamani na hata kwenye mapitio ya vitabu
vitakatifu yanaeleza juu ya jambo hilo. Kimsingi, hakuna tatizo katika
nguvu hiyo ya mwanaume. Katika kipindi hiki cha sayansi na teknolojia,
mambo yamebadilika kidogo na angalau mwanamke anapata nafasi mbalimbali
kwenye jamii.<br /><br />
Wanawake wa leo wanapewa vipaumbe kwenye uongozi wa
makampuni, taasisi, madhehebu ya dini, mashirika na vyama vya siasa na
serikali. Pamoja na yote hayo, bado mwanamke anabaki kuwa mwenye wakati
mgumu sana katika kufanya uamuzi au kujua hatma yake akiwa kwenye lindi
la mapenzi. <br /><br />
Anaweza kuwa mwanamke bora, mwenye msimamo na tija
kazini, lakini kwa mpenzi/mumewe anakuwa mpole asiyejua chochote
kitakachokuwa mbele yake.<br /><br />
Ni eneo ambalo mwanamke anakuwa hana
ujanja, hajiwezi na hajui cha kufanya, kwa sababu kila kitu kinachohusu
uhusiano kwake kinakuwa na giza nene mbele yake. Huu ni ukweli. <br /><br />
Ni
mada yenye ugumu kidogo kuingia akilini, lakini kichwa kikitulia na
kupitia kwa umakini mkubwa, mstari kwa mstari unaweza kuelewa vyema na
kubaki na kitu kipya kichwani mwako.<br /><strong> </strong><br />
<strong>NI NINI HASA?</strong><br />Ni
kuwa chini ya mamlaka ya mwanaume. Kuwa chini ya matakwa na kufuata
maelekezo. Wakati mwingine anaweza kupata nafasi ya kutoa mawazo yake,
lakini ni juu ya maisha tu – si mustakabali wa mapenzi yao.<br /><br />
Mwanamke
anaweza pia kutoa mapendekezo ya mapenzi yao, lakini hayawezi kuwa
uamuzi. Hata kama akitoa uamuzi, bado siri ya uhusiano huo inabaki kuwa
ya mwanaume. Mwanamke anaweza kuwa na upendo mkubwa, lakini akitegemea
zaidi sapoti ya mwanaume wake.<br />Kwa maneno mengine, hata kama ana
mapenzi yenye ukubwa gani, kama mwanaume wake atakuwa na uamuzi mwingine
ambao yeye haujui, yote yanaweza kuwa kazi bure mwisho wa siku.<br /><strong> </strong><br />
<strong>NI SAHIHI?</strong><br />Hakika.
Hakuna tatizo kwa mwanaume kuwa na mamlaka au uamuzi juu ya uhusiano
wake. Si kwamba yeye ndiye aliyejipangia mwenyewe bali ni utaratibu
alioukuta baada ya yeye kuzaliwa.<br />Mwanaume aliumbwa na kukabidhiiwa mamlaka moja kwa moja (mapitio ya vitabu Vitakatifu yanathibitisha hilo). <br /><strong> </strong><br />
<strong>KUNA ATHARI?</strong><br />Ndiyo!
Hapa ndipo kwenye msingi hasa wa mada yetu. Rafiki zangu, mamlaka ya
mwanaume yamekuwa machozi kwa wanawake wengi. Kwa sababu wanawake hawana
uwezo wa kujua kilichopo (hasa) ndani ya moyo wa mwanaume, wamekuwa
wakitumia mawazo na fikra tu.<br />Mwanamke anaweza kuupumzisha moyo wake
kwa mwanaume lakini akiwa hana uhakika wa nini kinachofuata, wakati
mwanaume anaweza kumpenda mwanamke na kuendelea kubaki na siri yake ya
nini kinachofuata ndani ya moyo wake. <br /><br />
Tunaona mengi <a class="skimwords-link" data-group-id="247339581" data-skim-creative="20204" data-skim-product="247339581" data-skimwords-id="247339581" data-skimwords-word="kila%20siku" href="http://www.amazon.co.uk/dp/B0096MJ3E2/" target="_blank" title="Shopping link added by SkimWords">kila siku </a>kwenye jamii yetu. Mwanamke anafanya jambo kwa msingi wa kumfurahisha
mpenzi wake, akiwa ameweka athari/mateso ambayo anaweza kuyapata kwa
furaha ya muda kwa mpenzi wake.<br />
<br />
Hata hivyo kipo kitu cha kufanya
rafiki zangu. Kuwa chini ya himaya ya mwanaume hakukunyimi haki ya
KUTAMBUA THAMA NI YAKO na NGUVU YA KUFIKIRI ILIYO NDANI YAKO. Bado
mwanamke anaweza kuendelea kuwa mwenye mipango na kuamini kwamba nguvu
ya ubongo wake ni kubwa kuliko hata mpenzi wake.<br /><br />
Kipo kitu cha
kufanya, lakini ili kukufanya uelewe vizuri zaidi mada yenyewe, hebu
twende tukaone matatizo wanayokutana nayo wanawake kutokana na kuacha
nguvu ya MAMLAKA ya mwanaume ifanye kazi na kushindwa kutumia uwezo wa
KUFIKIRI uliopo ndani yao. <br /><strong> </strong><br />
<strong>SUALA LA MIMBA</strong><br />Kupata
mimba kabla au nje ya ndoa ni tatizo. Ni jambo moja linalowahusu watu
wawili lakini likiwa ndani ya uamuzi wa mwanamke. Mimba si bahati mbaya.
Wanawake wanajua hili vizuri sana.<br />Wakati mwingine, wapenzi wanaweza
kuwa wamepima ukimwi na hivyo wana uhuru wa kuamua kukutana kwa kutumia
kinga au lah, lakini bado kuna suala la mimba ambalo linaweza
kumgharimu mwanamke huyo.<br /><br />
Ukiacha hilo, inatokea mwanaume
anamlazimisha mwanamke abebe mimba kwanza (eti) ndiyo atapeleka barua ya
posa kwao. Inawezekana mwanaume huyo ana lengo hilo, lakini kwa nini
alazimishe iwe kabla ya ndoa?<br /><br />
Kwa sababu sasa wanawake wengi huwa
wanaacha nguvu yao ya kufikiri, wanajikuta wameingia mkenge! Mwisho
jamaa anaingia mitini, mwanamke anabaki na mtoto wake. <br />Kwa nini
uache hili litokee? Kwani hujui namna ya kujikinga na mimba? Ukiachana
na kinga, kuna hata njia rahisi ya kuhesabu mzunguko wa mwezi, pia
hujui? Nafasi yangu kwa leo imeisha. Hadi wiki ijayo kwa mwendelezo
wake.<br /><strong> </strong><br />
<strong>Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya Mapenzi
anayeandikia Magazeti ya Global Publishers, ameandika vitabu vya True
Love, Let’s Talk About Love na All About Love vilivyopo mitaani</strong><br />
<br />
<strong><span style="font-weight: normal;">Habari hii ni kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers </span></strong></div>
Unknownnoreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-32451299786517805202012-10-20T18:47:00.002-07:002012-10-20T23:44:41.043-07:00Faida na hasara ya Sweet, Baby.. kwenye Mapenzi<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<div class="postbody">
<div class="xg_user_generated">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://2.bp.blogspot.com/-9U_sfXbnHFs/UIOZxtGnZDI/AAAAAAAABeg/tfEgWNowJiw/s1600/Beach+sex.png" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="640" src="http://2.bp.blogspot.com/-9U_sfXbnHFs/UIOZxtGnZDI/AAAAAAAABeg/tfEgWNowJiw/s640/Beach+sex.png" width="448" /></a></div>
<br />
<a href="http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/unajua-athari-za-kuitana-sweet-dear-baby#" id="_GPLITA_0" style="text-decoration: underline;" title="Click to Continue > by Text-Enhance">BABY</a>
ni neno la Kiingereza lenye maana ya mtoto, tena mara nyingi linatumika
kwa mtoto mdogo. Pia lina maana nyingine ya mpenzi. Ni neno maarufu
sana siku hizi; hata wazee kabisa, utasikia wanaitana baby!<br />
Mbali na hilo, yapo maneno mengine kama sweet, dear, <a href="http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/unajua-athari-za-kuitana-sweet-dear-baby#" id="_GPLITA_1" style="text-decoration: underline;" title="Click to Continue > by Text-Enhance">honey</a>
na mengine mengi. Maneno yote hayo ya Kiingereza, yana maana zaidi ya
moja, lakini kubwa zaidi ni kumaanisha mpenzi, mpendwa (hutumika katika
kuonesha mapenzi ya dhati kwa mwingine).<br />
Leo nataka kukupa kitu kipya
kabisa kichwani mwako. Unahitaji utulivu wa hali ya juu ili kujifunza
hili. Ni maneno mazuri sana, ya kipekee lakini kwa upande mwingine ni
hatari kwa sababu hukaribisha matatizo ambayo hayakutarajiwa na
mtumiaji.<br />
HUTUMIKA WAPI HASA?<br />
“Dear, naomba uniamshe saa 12:00
asubuhi, kesho nina vikao vingi sana asubuhi,” inaweza kuwa kauli ya
mume akimwambia mkewe, ambaye naye anamjibu: “Sawa <a href="http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/unajua-athari-za-kuitana-sweet-dear-baby#" id="_GPLITA_2" style="text-decoration: underline;" title="Click to Continue > by Text-Enhance">sweet</a>, usijali.”<br />
Kwa
hakika ndipo sehemu sahihi zaidi kutumika. Ni maneno yenye mshawasha
mkubwa na huonesha penzi la dhati lililopo moyoni mwa mhusika kwenda kwa
mpenzi wake.<br />
Husisimua na kuongeza ladha ya mapenzi ya kweli.
Kumuita mpenzi wako kwa majina ya kimapenzi huongeza zaidi upendo na
msisimko wa moyo. Mwenzi hujiona wa kipekee na mapenzi huzidi kukua.<br />
Kwa
maana hiyo basi, ni sahihi zaidi kwa wapenzi kuitana majina niliyotaja
hapo juu na mengine yanayofanana na hayo kwa lugha yoyote ile, ila iwe
inatambulika vizuri na anayetamkiwa.<br />
ATHARI SASA!<br />
Kwa upande
mwingine kuna athari za kutumia maneno hayo. Zama hizi, maneno hayo
yanaonekana ya kawaida tu. Mtu yeyote anaweza kumuita yeyote mpenzi,
honey, baby n.k. Hapo ndipo kwenye tatizo lenyewe.<br />
Kwa ujumla
wanawake ndiyo wanaongoza zaidi kuitana majina hayo. Wakati mwingine
huenda mbali zaidi na kuwaita hata wanaume majina hayo ya kimapenzi. Si
rahisi kuona athari zake kwa haraka na moja kwa moja, lakini zipo na
wengi zimewasababishia matatizo. Ngoja tuone..<br />
HUPUNGUZA THAMANI<br />
Kama nilivyotangulia kusema awali, maneno <br />
niliyotaja
hapo juu husisimua na kuongeza mapenzi. Kwa kuyatumia vinginevyo, basi
kwa kiasi kikubwa huanza kukuathiri na kupunguza thamani ya neno
lenyewe.<br />
Kama unaweza kumwita mfanyakazi mwenzako dear, mtu wa jinsi
sawa na wewe sweet ni wazi hata utakapomuita mpenzi wako au wewe kuitwa
na yeye, halitakuwa na nguvu sana ya mapenzi kwa sababu ni neno
ulilolizoea kila wakati.<br />
HUKARIBISHA USALITI<br />
Wakati mwingine
unaweza kujikuta umeingia kwenye usaliti bila kutarajia. Veronica,
mfanyakazi wa saluni moja ya kiume iliyopo Sinza, Dar alitoa ushuhuda
ufuatao:<br />
“Mimi naishi na mchumba wangu, tuna mtoto mmoja mwenye miaka
mitatu. Nafanya kazi saluni. Tangu nimeanza hii kazi, nimejifunza
kutumia maneno matamu ya kumfurahisha mteja na wakati mwingine kumfanya
akupe tipu baada ya kumaliza kazi.<br />
“Kuna kaka mmoja nilizoeana naye
sana. Kama kawaida, huwa namkaribisha kwa kumuita dear au sweet. Wakati
nikiendelea kumfanyia scrub, mazungumzo yetu hutawaliwa na dear, sweet,
nikajikuta nimezidi kumzoea.<br />
“Kwa sababu tulibadilishana namba, mara
akaanza kuwa na mazoea ya kunitumia meseji, akija ananipa pesa,
anaondoka. Mazoea yakazidi. Nikajikuta nimemzoea na kuna siku ambayo
siwezi kuisahau kabisa.<br />
“Ni siku niliyomsaliti mchumba wangu...mbaya
zaidi na huyo jamaa naye ana mke wake. Niliumia sana, lakini naamini
kama nisingekuwa na mazoea ya kumuita majina ya kimapenzi nadhani
nisingeingia mtegoni. Moyo wangu unauma sana, najuta kumsaliti mpenzi
wangu.”<br />
Unaweza usione athari hii moja kwa moja, lakini ndugu zangu
chukua jambo hili leo; wanaume wengi wakiitwa kwa majina ya kimapenzi
husisimka sana – hujiona wenye bahati na mara hushawishika kuingia
mapenzi.<br />
Kama mwanamke hatakuwa makini atajikuta ametumbukia. Ya <a href="http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/unajua-athari-za-kuitana-sweet-dear-baby#" id="_GPLITA_4" style="text-decoration: underline;" title="Click to Continue > by Text-Enhance">nini</a> yote hayo, wakati unaweza kubadilisha mazoea hayo? <br />
ANGALIA TOFAUTI<br />
Rafiki zangu, <a href="http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/unajua-athari-za-kuitana-sweet-dear-baby#" id="_GPLITA_5" style="text-decoration: underline;" title="Click to Continue > by Text-Enhance">kati</a>
ya maneno niliyoyataja, kuna ambayo yanakubalika kutumiwa na wasio na
uhusiano lakini wawe na undugu wa damu. Mathalani baba, mama, kaka,
dada, shangazi nk.<br />
<a href="http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/unajua-athari-za-kuitana-sweet-dear-baby#" id="_GPLITA_3" style="text-decoration: underline;" title="Click to Continue > by Text-Enhance">Hakuna</a>
tatizo kumuita mtu mpendwa, lakini siyo baby, sweet, mpenzi na mengine
yenye maana ya moja kwa moja ya kimapenzi. Umenipata? Akili za kuambiwa,
changanya na zako kisha unazifanyia kazi! Chukua kinachokufaa!<br />
<br />
Habari hii ni kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers<br />
<br /></div>
</div>
</div>
Unknownnoreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-35920321819194040602012-10-20T18:22:00.000-07:002012-10-20T18:25:03.144-07:00Jifunze kumsifu Mpenzi wako akupe mazuri zaidi<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://2.bp.blogspot.com/-egg49NRQmDg/UINOzr6YYhI/AAAAAAAABb0/ZBwE72TOHHY/s1600/HOT+LOVE.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="640" src="http://2.bp.blogspot.com/-egg49NRQmDg/UINOzr6YYhI/AAAAAAAABb0/ZBwE72TOHHY/s640/HOT+LOVE.jpg" width="474" /></a></div>
<br />
YAPO mengi mazuri ambayo huenda mpenzi wako aliwahi kukufanyia, je
uliwahi kumshukuru kwa kukufanya ufarijike? Naamini Mungu amekujaalia
kuwa na mpenzi mzuri, mwenye kila sifa ambayo ulitamani awe nayo, je
ulishawahi kumsifia hata kwa kumwambia ni mzuri?<br />
Huenda ulishawahi
kufanya hivyo lakini kwa taarifa yako wapo ambao wanahisi kufanya hivyo
eti ni ulimbukeni. Ulimbukeni? Kumsifia mpenzi wako unaona ni
ulimbukeni wakati wataalam wa masuala ya mapenzi wanaeleza kuwa,
wanawake ni watu wanaopenda kusifiwa sana hata kwa madogo wanayoyafanya?<br />
Unaona
hatari gani kumsifia mpenzi wako kuwa ni mzuri? Unadhani unatumia nguvu
gani kumsifia mpenzi wako kutokana na mahaba mazito anayokupata? <br />
Kwa taarifa yako unaweza kuona ni kitu kidogo sana lakini madhara yake kwenye penzi ni makubwa.<br />
Kumsifia
mpenzi wako kwa yale anayokufanyia kuna faida nyingi sana lakini kwa
leo nitagusia chache. Kwanza kunaongeza mapenzi. Mume/mke anaposifiwa
kuwa anajua mapenzi hata kama si kwa kiwango kikubwa, anafarijika sana.<br />
Unapomwambia
mpenzi wako: ‘Dear nashukuru kwa mapenzi uliyonipa jana, umenipa furaha
ya ajabu ambayo siamini kama kuna mtu mwingine wa kunipa, nakupenda
sana’. <br />
Maneno kama haya hutumii nguvu wala muda mwingi kuyafikisha
kwa mpenzi wako lakini uzito wake ni mkubwa. Kwanza anajihisi
aliyekamilika kwa kufikia hatua ya kufanya mambo yakamridhisha mpenzi
wake na kwa mazingira hayo anaamini huwezi kumsaliti. Hisia hizo
zitamfanya azidi kukupenda.<br />
Hilo ni kwa wote yaani kwa mwanaume na
mwanamke. Lakini pia unapomsifia mpenzi wako kwa yale anayokufanyia,
unamfanya aongeze kasi ya kukufanyia ili nawe uzidi kumpenda. <br />
Kwa mfano, unapokutana na mpenzi wako kisha ukamwambia ‘umependeza kweli mpenzi wangu, nazidi kukupenda kwa unavyovaa’. <br />
Mtu
anayeambiwa maneno haya atajitahidi sana siku zote aonekane nadhifu na
wa kuvutia kwa mpenzi wake akijua kwamba, akivaa ilimradi kuvaa,
hatamfurahisha mpenzi wake. Kwa maana hiyo kumsifia mpenzi wako
kunamfanya azidi kuwa bora.<br />
Lakini kusifia kusiwe kwa kinafiki. Usimsifie mpenzi wako eti ili kumfanya ajione bora kumbe katika uhalisia siyo hivyo.<br />
Tusifiane
pale inapobidi huku tukijua kuwa kwa kufanya hivyo tutapata faida.
Tusiwe na tabia ya kuchukulia poa kila tunachofanyiwa na wapenzi wetu. <br />
Kama
kakuridhisha kimapenzi, msifie kwamba yeye ni muhimu kwako kwa kuwa
amekupa ulichotarajia. Amekupikia chakula kizuri, msifie kuwa yeye ni
mpishi mzuri. Hiyo italinogesha penzi na utashangaa kila siku
inayokwenda kwa Mungu penzi lenu linachanua.<br />
Lakini mbali na hayo,
unatakiwa kuridhika kwa kile unachokipata kutoka kwa huyo mpenzi wako
ulinaye kwa sasa. Najua kwenye uhusiano wengi tumetoka mbali. Wapo
waliowahi kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja huko nyuma na kila mmoja
alikuwa na kiwango chake cha kukuridhisha. <br />
Inawezekana kuna ambaye
unamkumbuka kwa mapenzi mazito aliyokuwa anakupa zaidi ya huyo
uliyenaye. Hiyo ni historia, imepita! Kama huyo uliyenaye si mtaalam
sana wa kukufikisha pale unapopata, ridhika na hicho kidogo unachokipata
endapo atakuwa anaonesha kukupenda kwa dhati.<br />
Mpe moyo, msifiesifie kidogo kwa hiyo furaha kiduchu anayokupa huku ukiamini kuwa, atabadilika kadiri siku zinavyokwenda.<br />
Kumbuka
cha msingi katika maisha yetu ni kumpata mtu mwenye mapenzi ya kweli na
si kumpata anayeweza kukuridhisha katika mambo kadha wa kadha.<br />
<br />
Habari hii ni kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers </div>
Unknownnoreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-33064129955182283972012-10-20T17:23:00.003-07:002012-10-20T23:41:10.844-07:00Wanaume mnajua hili: Mfanyie mwanamke akuzidishie raha<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://4.bp.blogspot.com/-IU44qwr2pxo/UINB00qFnWI/AAAAAAAABbk/NtlC1r1Ntg0/s1600/SEXST.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="640" src="http://4.bp.blogspot.com/-IU44qwr2pxo/UINB00qFnWI/AAAAAAAABbk/NtlC1r1Ntg0/s640/SEXST.jpg" width="480" /></a></div>
MAMBO vipi ndugu zangu? Ni furaha yangu kwa mara nyingine tena kukutana
nanyi wapendwa wasomaji wa safu yetu hii. Tumshukuru Muumba wetu kwa
kutujaalia uhai na afya njema, lakini zaidi ya hapo tumshukuru pia kwa
kutuumbia kitu mapenzi au siyo jamani?<br />
Siku zote hatutaacha kuzungumza juu ya mapenzi kwani ni ukweli usiopingika kwamba mapenzi ndiyo maisha yetu. <br />
Tunafanya
kazi usiku na mchana, tunahangaika huku na huko, lakini mwisho wa siku
tunafikiria jinsi gani tutapata kuboresha na kufurahia maisha na wapenzi
wetu. <br />
Tunafikiria pia ni jinsi gani tunaweza tukapata utulivu na
amani katika maisha ya kimapenzi na wapenzi wetu, waume zetu au wake
zetu katika siku zote za maisha yetu.<br />
Ndugu zangu, Mungu ametuwekea mapenzi ili tupate raha na amani katika maisha yetu.<br />
Kwa
maana hiyo, wale wanaoyachezea na kuyavuruga mapenzi kwa makusudi kwa
kuumiza hisia za wenzao kisha kuwasababishia vilio si watu wa kupendeza
mbele ya macho ya wale wanaojua hasa nini maana ya mapenzi. <br />
Wanawake
ni watu wa kuheshimika na kupewa furaha wanayohitaji. Unapompata
mwanamke anayekupenda na kukuheshimu, huna sababu ya kumfanya ajute kuwa
na wewe. <br />
MPENDE NA MTHAMINI!<br />
Yawapasa wanaume mfahamu kuwa,
wanawake ni zawadi kwenu, pumziko na tulizo la mioyo yenu. Wanawake
ndiyo raha na amani kubwa ya maisha yenu.<br />
Kosa kubwa mnalofanya
wanaume ni kuutumia vibaya mfumo dume hasa katika suala nyeti kama
mapenzi. Mapenzi si ubabe, mapenzi ni upole na ukarimu. <br />
Pamoja na
kwamba mmebarikiwa kwa kupewa nafasi ya kuwa kichwa katika nyumba lakini
linapokuja suala la kurekebisha tofauti zinazojitokeza katika uhusiano
wenu, si vyema kutumia njia za kibabe.<br />
Niwaambie kitu, wanawake ni wa
hisia zaidi na waliobarikiwa kuwa na upendo wa hali ya juu na ndiyo
maana wakapewa dhamana ya kubeba mtoto tumboni kwa miezi tisa na pia
kumnyonyesha na kumlea kwa miaka kadhaa, wewe mwanaume ungeweza?<br />
Nasema
ni watu wa hisia kwa sababu, hivi uliwahi kufikiri ni kwa nini wanawake
huridhika na kujisikia poa kweli wanapopewa zawadi kama ya maua na kadi
zenye ujumbe wa mapenzi ukilinganisha na wanaume? <br />
Unafikiri ni kwa
nini wana machozi ya haraka wanapotendwa? Au unafikiri ni kwa nini
wanapenda kutumiwa ‘love sms’ zaidi kuliko kupigiwa simu? Jiulize.<br />
Mimi
nawaona wanawake kama watu wa kuheshimiwa na kupendwa kwa dhati.
Mkumbuke wanawake ndiyo mama zetu, walezi wetu na ndiyo nyumba zetu.
Jaribuni pia kujicontroo na huo mnaouita ukijogoo kwamba eti ninyi ni
watu msioridhika na mpenzi mmoja. <br />
Jaribuni kufanya kila mnaloweza
kuifuta ile dhana ya kwamba wanaume hawaaminiki hata kidogo. Ridhika na
mpenzi uliyenaye, heshimu hisia zake na thamini mapenzi yake kwako na
mpe ile kitu roho inapenda!<br />
Ni hayo tu kwa leo.<br />
<br />
Habari ni kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers </div>
Unknownnoreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-3488960203075303385.post-31141840441163948302012-10-20T15:47:00.000-07:002012-10-20T19:24:09.152-07:00Kauli Zenye Ishara Mbaya katika Mapenzi<div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
</div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<a href="http://2.bp.blogspot.com/-OYtMvxmLrpY/UINcoiWpEHI/AAAAAAAABdI/mSHo9oe39mk/s1600/hotsex.png" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" height="640" src="http://2.bp.blogspot.com/-OYtMvxmLrpY/UINcoiWpEHI/AAAAAAAABdI/mSHo9oe39mk/s640/hotsex.png" width="502" /></a></div>
<br />
MATARAJIO YA wengi katika uhusiano ni kuwa na furaha, hakuna
kinachotafutwa katika mapenzi zaidi ya faraja ya moyo. Lakini ili uweze
kuipata ni lazima kuwe na mapenzi ya dhati.<br />
Vichwa vya wengi walio
katika uhusiano ni kusaka penzi la dhati! Hakuna anayependa kunyanyasika
au kuwa na mashaka na mpenzi wake. Katika hili lazima uwe makini sana,
maana unaweza kuwa katika uhusiano na mwenzi ambaye ‘yupoyupo’ tu na
wala hana mpango wowote na wewe, lakini wewe ukawa hujui.<br />
<br />
Kwa bahati mbaya sana, baadhi ya marafiki zangu, wanashindwa kuchuja
pumba na nafaka kwa sababu wakati wanafanya uchaguzi hawakuzingatia
vigezo.<br />
Vijana wengi wa siku hizi, huzingatia zaidi mwonekano wa nje,
jambo ambalo ni baya kwani mwonekano wa nje, hauwezi kukuonesha mabaya
ya mpenzi wako hata siku moja. <br />
Kama ulichagua mwezi kwa kuzingatia
tabia na mambo mengine ya msingi, ni rahisi zaidi kwako kugundua penzi
ulilonalo ni la dhati au lile la ‘nataka pochi lako tu!’<br />
Pointi ya
msingi hapa ni lugha zenye ishara mbaya kwa wapenzi. Umewahi kujiuliza
kuhusu hili? Umewahi kutafakari juu ya kauli chafu anazotoa mpenzi wako
dhidi yako?<br />
Yaani unashangaa mwenzi wako anakuwa mtu wa kutoa kauli
za maudhi, kashfa na hata matusi wakati mwingine. Wewe unazichukuliaje?
Rafiki zangu, kauli ya mtu inaweza kukutoa gizani na kugundua ukweli
uliopo ndani yake, lakini kama hutakuwa makini, unaweza kuchukulia kama
utani na kuuacha ukweli uendelee, mwisho unakuja kushtuka, umeshaachwa!<br />
Hapa
nimekuandalia kauli zenye ishara mbaya ya penzi lako. Ukiona moja kati
ya kauli zifuatazo, basi kuwa na mashaka, kisha fanyia kazi, utagundua
ukweli.<br />
<b>HUVUTII!</b><br />
Kati ya kauli mbaya zaidi katika
uhusiano ni pale mpenzi wako atakapokuambia huna mvuto! Haijalishi
amekuambia akiwa katika hali gani; utani au akimaanisha, lakini neno
hilo si zuri kuambiwa na mpenzi wako.<br />
Kuambiwa huvutii, katika
mapenzi ni tusi kubwa. Nini maana ya mvuto basi? Nani umvutie? Ni wapita
njia? Ofisini? Sokoni? Ana maana gani hasa?...<br />
Siku zote mvuto ni
kwa ajili ya mpenzi wako, ndiyo maana mkawa katika uhusiano, hii
inamaananisha ulimvutia ndiyo sababu akakukubali. Kukuambia huvutii si
utani, ni kweli haoni mvuto na inawezekana penzi limeshachuja. <br />
Inawezekana
akawa anafanya mzaha, kama ndivyo, atasoma ulivyopokea, akiona
umekasirika atarekebisha usemi wake haraka, kama ni vinginevyo
ataendelea kushikilia msimamo wake, hata kama ni kwa utani, lakini
atakuwa anakufikishia ujumbe wako kwamba huna mvuto, kwa maneno mengine
humvutii, humfai; kwa hiyo muachane. Kuna nini tena hapo? Akili kichwani
mwako.<br />
<b>HUPENDEZI!</b><br />
Hii ni kauli nyingine mbaya.
Unapoambiwa: “Hujapendeza kabisa, yaani huna uwezo wa kupangilia nguo,
kila siku unachemsha!” ujue kuna hatari hapo, angalia mara mbili
uhusiano wenu.<br />
Kuambiwa hujapendeza kunashusha thamani yako na
kuonekana huna ujanja wa kufanya uchaguzi mzuri wa mavazi. Huenda ni
kweli hujapendeza, lakini hilo si la kubeza. <br />
Anatakiwa kukuambia kwa
upole namna ambavyo unatakiwa kuvaa na kuonekana nadhifu. Kwa maneno
mengine, kukuambia hujapendeza ni kama anakusuta, hakukubali na
unamuaibisha! <br />
Rafiki yangu mpenzi, bado kuna mengi ya kujifunza
zaidi lakini kutokana na ufinyu wa nafasi yangu, naomba niweke kituo
kikubwa hapa.<br />
<br />
Habari ni kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers </div>
Unknownnoreply@blogger.com0